Na Esther Macha, Timesmajira Online,Mbeya
MBUNGE wa Jimbo la Songwe ,Philipo Mulugo amefika jijini Mbeya kushiriki na kuaga miili ya watu wanne waliofariki kwenye ajali akiwemo mwandishi wa habari na mpiga picha wa TBC Furaha Simchimba.
Watu hao waliofariki katika ajali iliyotokea Februari 25,2025 iliyohusisha gari la kampuni ya CRN Safari na gari la Serikali aina ya Land Cruiser.
Mulugo akitoa salamu hizo pia amekabidhi rambirambi kwa familia nne zilizopoteza wapendwa wao katika ajali hiyo .
Waliofariki katika ajali hiyo ni pamoja na Daniel Mselewa, Thadeo Thadeo, Isaya Geazi na Furaha Simchimba.
More Stories
RC Chalamila kushuhudia mapambano 14 KnockOut ya Mama
Mfuko wa Utamaduni na Sanaa Tanzania wajivunia ongezeko bajeti ya bil.3 miaka minne ya Dkt.Samia
Khimji kumchangia Zungu fomu ya Ubunge