📌 Azungumzia suala la magari ya Serikali kufungwa mfumo wa CNG
Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania ( TPDC), inajenga vituo vya kujazia gesi kwenye magari (CNG) mkoani Dar es Salaam (viwili) na mkoani Pwani (kimoja) huku TPDC ikiendelea na ununuzi wa vituo vidogo vya kujaza CNG kwenye magari vinavyohamishika ambavyo vitasimikwa katika mikoa ya Dar es Salaam (vitatu), Morogoro (kimoja) na Dodoma ( viwili).
Mhe. Judith Kapinga amesema hayo tarehe 27 Agosti, 2024 bungeni jijini Dodoma wakati wa kipindi cha Maswali na Majibu.

Amesema kwa sasa kuna vituo vitano vya kujazia gesi kwenye magari katika mikoa ya Dar es Salaam (Ubungo Maziwa, Tazara na Uwanja wa Ndege), Pwani (Mkuranga) na Mtwara (Dangote).
Kuhusu mpango wa magari ya Serikali kutumia mfumo wa CNG amesema kuwa tayari Mtaalam Mshauri ameshapatikana lengo likiwa ni kuhakikisha kwamba suala hilo linafanyika kwa ufanisi.

More Stories
Utafiti wafichua mazito sekta ya uvuvi baharini
Takwimu Rasmi kuongoza utekelezaji Dira 2050
TBS kuadhimisha miaka 50,kuzindua kitabu chake