
Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
Tigo na ZMotion wametoa mafunzo ya mfumo wa malipo ya Ada kwa wamiliki wa shule binafsi Tanzania kuwa mfumo wa ‘LIPA ADA’ ni mojawapo ya ubunifu wa kiteknolojia uliolenga kutatua changamoto zinazowakumba wazazi na shule katika suala la ulipaji ada.
Aidha, Malipo kwa kupitia mfumo huo yatakuwa yakifanyika kupitia huduma ya TigoPesa, hivyo kurahisisha mchakato mzima.
Mafunzo hayo yamefanyika Jijini Dar es Salaam, yakiwa na lengo la kuhakikisha ufanisi wa mfumo huo mpya ambao unatoa fursa kwa wazazi kulipia ada kidogo kidogo kulingana na uwezo wao ambapo mafunzo hayo yametolewa kwa siku moja kwa wamiliki na wakurugenzi wa shule binafsi kuhusu huduma yetu mpya ya LIPA ADA.
Naye, Mkurugenzi wa Biashara-Tigo Pesa, James Sumari, alieleza kuwa mfumo wa ‘LIPA ADA’ ni mojawapo ya ubunifu wa kiteknolojia uliolenga kutatua changamoto zinazowakumba wazazi na shule katika suala la ulipaji ada.
Hivyo, Mkurugenzi wa ZMotion Said Ally amebainisha kuwa mfumo wa ‘LIPA ADA’ umesanifiwa kwa kuzingatia mahitaji ya shule binafsi na ni rahisi kutumia

More Stories
Wapambe waanza rafu za uchaguzi Morogoro Mjini
Daraja la J.P.Magufuli kuzinduliwa Juni 19,2025
Yas yazidi kuboresha huduma sekta ya Utalii