September 21, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Kamishna Mkuu TRA akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu TPA

Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Yusuph Mwenda amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Bw. Plasduce Mbossa.

katika mazungumzo hayo walijadili namna ya kuboresha uhusiano wa TRA na TPA na kuendelea kufanya kazi kwa pamoja na kwa karibu zaidi ili kuimarisha utendaji kazi kwa taasisi zote mbili.


Kikao hicho kimefanyika leo tarehe 31.07.2024
katika ofisi Kuu za TPA jijini Dar es Salaam.

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Yusuph Mwenda (wa kwanz akushoto) akifanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Plasduce Mbossa (Kulia) wakijadili namna ya kuboresha uhusiano wa TRA na TPA na kuendelea kufanya kazi kwa pamoja na kwa karibu zaidi ili kuimarisha utendaji kazi kwa taasisi zote mbili. Kikao hicho kimefanyika leo tarehe 31.07.2024 leo katika ofisi Kuu za TPA jijini Dar es Salaam.
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Yusuph Mwenda akisalimiana na Naibu Waziri wa Uchukuzi Mh. David Kihenzile walipokutana katika kikao kati ya Kamishna Mkuu wa TRA na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Bw. Plasduce Mbossa kilichofanyika leo katika Ofisi za TPA, jijini Dar es Salaam.