October 6, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

TANESCO yatoa elimu matumizi bora ya umeme migodini Mbeya

Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online, Mbeya

MaafisaTANESCO wakipata maelezo kutoka kwa Afisa madini wa kiwanda Cha Mdimi investment kilichoko wilayani Chunya mkoani Mbeya Joseph Mamuya wakati maafisa hao walipotembelea kiwandani hapo jana.

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) kupitia idara ya masoko, limeendelea na kampeni kabambe ya kuhakikisha inatoa elimu kwa wachimbaji wadogo, kati na wakubwa wa madini pamoja na mashine za kusaga nafaka mkoani mbeya ili wafahamu elimu ya matumizi Bora ya umeme.

Lengo la kampeni hiyo Ni kuhamasisha matumizi bora ya umeme, usalama wa umeme kwa viwanda hivyo, kuunga mkono jitihada za Mh Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuhakikisha uchumi wa viwanda unafikiwa kwa Kasi nchini na kuongeza Tija kwa Taifa.

Miongoni mwa migodi ambayo imekwishatembelewa mkoani Mbeya ni pamoja na mgodi wa makaa ya Mawe Kiwira, mgodi wa dhahabu Chunya wa Mdimi investment, Mehrab minerals resources, mgodi wa mama Today iliyoko wilayani Chunya.

Vijana kutoka kiwanda Cha kuchakata mbao kutoka Tukuyu Cha Kapinga wakisikiliza kwa making Elimu inayohusu masuala ya umeme wakati walipowatembelea
Maafisa wa TANESCO wakiwa kwenye moja ya viwanda walivyotembelea