Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Qatar nchini Mhe. Hussain Ahmad Al – Homaid katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo yao, viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali hususani ya kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Qartar ambapo Balozi Fatma amemhakikishia Balozi wa Qatar kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Qatar kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo viwanda, biashara na uwekezaji.
More Stories
Mtwange:Mradi wa kuzalisha umeme wa jua Kishapu wafikia asilimia 63.3
Ussi awataka wananchi Handeni kulinda miundombinu ya maji
Wapambe waanza rafu za uchaguzi Morogoro Mjini