Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Qatar nchini Mhe. Hussain Ahmad Al – Homaid katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.
Katika mazungumzo yao, viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali hususani ya kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Qartar ambapo Balozi Fatma amemhakikishia Balozi wa Qatar kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Qatar kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo viwanda, biashara na uwekezaji.
More Stories
Naibu Waziri Sangu aitaka e-GA kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi
Dkt.Tulia avitaka vikundi vya ngoma vilivyoshinda kubadilisha maisha yao
Rais Samia ahutubia zaidi ya wananchi 30,000 waliofurika uwanja wa majimaji Songea Ruvuma