Na Joyce Kasiki,TimesMajira Online,Dodoma
Mbunge wa Viti Maalum kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Rhoda Kunchela amesema, yeye kama Mbunge ni wajibu wake kukichangia chama, kwani chama kinatumia fedha kwa ajili ya kujiendesha.
Ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutoka kwenye mahojiano ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) jijini Dodoma.
Amesema,michango ya chama ipo kikatiba na kuchangia ni lazima na siyo ombi wala hiyari, kwani fedha zilizolalamikiwa na wabunge zinafanya kazi nzuri ya kuimarisha chama.
Kunchela amesema,matumizi ya fedha hizo yanaonekana kwa vitu mbalimbali vinavyonunuliwa na operesheni za chama zinazofanyika nchini kote.
More Stories
Prof.Muhongo awakaribisha wadau kuchangia ujenzi maabara masomo ya Sayansi
Serikali yakaribisha wawekezaji sekta ya madini
Matindi: Ufanisi utaleta matokeo chanya sekta ya anga