Na Joyce Kasiki,Timesmajira online,Dodoma
WAZIRI wa nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Jenista Mhagama amewataka watumishi wa Umma kufanya Kazi kwa kujituma kwa maslahi mapana ya Taifa.
Akizungumza na watumishi wa Wizara hiyo Mhagama amesema,endapo watumishi wakifanya Kazi vizuri inamUhamasisha Rais Samia Suluhu Hassan kujibu hoja zinazowakabili watumishi wa Umma kwa vitendo.
“Zawadi pekee kwa watumishi wa Umma ya kumpa Rais (Samia Suluhu Hassan) ni kiwajibika kwa vitendo…,unajua kadri tunavyokuwa tunawajibika tunampa hamasa Rais kujibi hoja za watumishi wa Umma kwa vitendo.”amesema Waziri Mhagama na kuongeza kuwa
“Mimi natamani mtumishi wa Umma aipende Kazi hadi siku akikosa kwenda kazini akipimwa akutwe’ temperature'( joto) imepanda.”

More Stories
Bilioni 7 kuwainua vijana 308 sekta ya uvuvi
Clara:Miaka 50 ya Sabasaba fursa mpya za Biashara na Uwekezaji
Usajili wa Laini za Simu: Jilinde Dhidi ya Kutumiwa Vibaya kwa Utambulisho Wako