Na Mwandishi wetu,timesmajira,Online
JESHI la Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam, linamshikilia mtu mmoja mwenye umri wa miaka 16 kwa madai ya kumlawiti mtoto wa miaka 4 na kusababisha kifo.
Kamanda wa Polisi Kanda hiyo, ACP Muliro Muliro amesema jana kuwa tukio hilo lilitokea Novemba 10, 2021 majira ya saa tatu asubuhi , Chamanzi Mbande Wilaya ya Temeke.
Amesema uchunguzi wa kina juu ya tukio hilo unafanyika na hatua za kisheria wakati wa uchunguzi zitazingatiwa  ili itendeke pande zote mbili.

More Stories
Serikali kuendelea kupanua fursa elimu Singida
Kumekucha CDF Cup 2026, NMB yaweka Sh milioni 150
TISEZA Songea kuvutia uwekezaji, ajira zaidi zapatikana