Na Mwandishi Wetu, TimesMajira online
MSANII wa muziki na Mjasiriamali hapa nchini Zuwena Mohamed maarufu kama ‘Shilole’, ameweka wazi kuwa amefunga ndoa na aliyekuwa mchumba wake wa hivi karibuni Rajab Issa maarufu ‘Rommy’ kwa ajili ya kumpendeza mwenyezi Mungu.
Akiweka wazi hilo, Kupitia kwenye ukurasa wake wa Instagram jana, Shilole ameshukuru mara baada ya kufunga ndoa na kusema wamemaliza salama ambapo kwa sasa anaitwa Mrs Rommy.
“Alhamdulillah tumemaliza salama, rasmi ni mume na mke niliechukuliwa kwa furaha na upendo wa juu ‘Officially Husband and Wife happily taken and very much in love’ kwasasa unaweza kuniita Mrs Rajab Issa (Rommy) Yarabbi iwe salama,” ameandika Shilole.
Kabla ya hapo Shilole alikuwa kwenye ndoa na mfanyabiashara Uchebe na waliachana mwaka jana baada ya ugomvi mkubwa uliotokea kwenye ndoa yao.
More Stories
Tamasha la utamaduni mkoani Ruvuma lapamba moto, Rais Samia mgeni rasmi
TANAPA yazindua Twenzetu Kilele msimu wa nne
Shamrashamra maadhimisho ya miaka 60 JWTZ yaendelea