Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online-Dar
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Dkt. Ngwaru Maghembe,amefanya mazungumzo na Balozi wa Cuba nchini Tanzania,Yordenis Despaigne Vera, katika ofisi ndogo za Wizara hiyo , jijini Dar-es-Salaam.
Mazungumzo hayo yamefanyika Februari 10,2026,yakilenga kujadiliana namna ya kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia baina ya Tanzania na Cuba.

Ikumbukwe kuwa,Tanzania na Cuba zimekuwa na uhusiano wa karibu na kindugu zaidi ya miongo sita iliyopita ambapo nchi hizo mbili zilianzisha ushirikiano wa kidiplomasia mwaka 1962.
Uhusiano huo umejengwa tangu enzi za kupigania uhuru ambapo viongozi waasisi wa mataifa hayo Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere wa Tanzania na Hayati Fidel Castro wa Cuba, ambao walijenga msingi wa uhusiano, usawa na maendeleo ya pamoja.
Kwa pamoja viongozi hao, wamejadiliana namna bora ya kuendeleza ushirikiano wa uwili na kimataifa kwa maslahi ya pande zote mbili.



More Stories
Wanawake jumuia ya kikristo Tanzania CCT wafundana kuelekea siku ya Wanawake Duniani
Dkt.Tulia,Mwalunenge waungana kutatua changamoto ya barabara
TUCASA yaomba kuanzishwa sheria malipo sekta ya ujenzi