March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Prof. Mapesa atembelea ujenzi wa Kafteria MNMA Kampasi ya Karume Zanzibar

Na Mwandishi wetu,Timesmajira

Mkuu wa Chuo cha kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Prof. Haruni Mapesa leo ametembelea eneo la mradi wa ujenzi wa Kafteria katika chuo cha kumbukumbu ya mwalimu Nyerere kampasi ya Karume Zanzibar ili kujionea nanna shughuli za ujenzi zinavyoendelea

Katika ziara hiyo ya kiutendaji, Prof. Mapesa pia amepokea ripoti ya ujenzi wa kafteria hiyo kutoka kwa kamati ya ujenzi.

Aidha pamoja na ukaguzi huo alipata fursa ya kuhudhuria kikao cha maandalizi ya mahafali ya 10 ya kampasi ya karume yanayotarajiwa kufanyika hivi karibuni.