Na Heri Shaaban, Timesmajira Online,Ilala
MWENYEKITI wa Serikali ya Mtaa wa Karume wilayani Ilala jijini Dar,Hajji Bechina,ametoa chakula kwa ajili ya sikukuu ya Eid kwa wananchi 560 vyenye thamani ya milioni 10.
Akizungumza katika tukio hilo Bechina,amesema ametoa sadaka hiyo kwa wananchi na makundi maalum.Ambapo kila mwaka amekuwa alifanya hivyo
Sanjari na hayo alikabidhi runinga ya inchi 46 kwa vijiwe viwili vya Young Star na Wachonga vinyango vyote vya Ilala,huku akiwahimiza wananchi kuchagua wagombea wanaotokana na Chama Cha Mapinduzi(CCM), katika uchaguzi mkuu unatarajiwa kufanyika mwaka huu.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya Ilala, Said Sidde,amewahimiza Wenyeviti na viongozi wengine kuiga mfano wa Mwenyekiti huyo wa kuwajali wananchi wake.
More Stories
Mwongozo wa kitaifa kwa watoa huduma za maendeleo ya biashara wazinduliwa
Zanzibar ipo tayari kupokea wawekezaji wa ndani na nje ya nchi
Elimu ya kilimo tija yawafikia wakulima mikoa mitano.