April 16, 2025

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Watumishi Bodi ya Barabara watakiwa kuzingatia uadilifu

Na Judith Ferdinand 

Watumishi wa Bodi ya Mfuko wa Barabara(RFB),wametakiwa kuwa wazalendo na kuzingatia uwajibikaji na uadilifu katika maeneo yao ya kazi,ili kuchochea maendeleo ya bodi na taifa kwa ujumla.

Wito huo umetolewa na Kaimu Mtendaji Mkuu Mfuko wa Barabara Mhandisi Rashid Kalimbaga, Aprili 14,2025,mkoani Morogoro katika kikao kazi cha siku tatu kilicholenga kuleta mabadiliko katika utendaji kazi.

Kaimu Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Barabara Mhandisi Rashid Kalimbaga akifungua kikao kazi cha ndani cha wafanyakazi wa Bodi ya Mfuko wa Barabara kinachofanyika mkoani Morogoro.

Huku akiwataka watumishi hao kushirikiana na Idara ili kuleta mabadiliko chanya katika maeneo ya kazi kwa ajili ya kuyafikia malengo waliyojiwekea.

Sanjari na hayo Mhandisi Kalimbaga,amesema  katika kikao hicho mada mbalimbali zitatolewa ikiwemo elimu ya utunzaji wa siri za Serikali,elimu kuhusu afya ya akili pamoja na masuala ya utumishi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali Watu na Utawala kutoka Bodi ya Mfuko wa Barabara, Aureus Mapunda amesema kikao hicho kitawasaidia watumishi kujikumbusha katika shughuli wanazozifanya mahala pakazi huku wakitarajia baada ya kikao hicho utendaji kazi wa mfuko huo utaboreka zaidi.

Mkurugenzi wa Idara ya Mipango na Mapato wa Bodi ya Mfuko wa Barabara Godlove Stephen, akifafanua jambo wakati wa kikao cha ndani cha Bodi hiyo kinachofanyika kwa siku tatu mkoani Morogoro

Nae Hindu Mussa ambae ni mmoja kati ya Watumishi wa Bodi ya Mfuko wa Barabara, amesema,kikao hicho kitawawezesha watumishi wote kukumbukan wajibu wao kama Watumishi wa Umma lakini pia kukabiliana na changamoto mbalimbali za kimaisha ikiwemo magonjwa ya afya ya akili.

Dr. Garvin Nathaniel Kweka kutoka Hospital ya Taifa ya Muhimbili akiwasilisha mada mbalimbali wakati wa kikao kazi cha ndani cha Wafanyakazi wa Bodi ya Mfuko wa Barabara kinachofanyika kwa siku tatu mkoani Morogoro
Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Barabara Mhandisi Rashid Kalimbaga,(katikati)akiwa kwenye picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Bodi ya Mfuko wa Barabara, mara baada ya kufungua kikao kazi cha ndani cha Bodi hiyo, kinachofanyika kwa siku tatu mkoani Morogoro