Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online,Zanzibar
WANAWAKE Wahasibu wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wameshiriki kongamano la kitaaluma la wanawake wahasibu linalofanyika katika hotel ya Verde Zanzibar.

Kongamano hilo la nne limefunguliwa jana na Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Hemed Suleiman Abdallah akimwakilisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi,Dkt.Hussein Ally Hassan Mwinyi.
TANESCO imefadhili kongamano hilo lengo likiwa ni kuwakutanisha wahasabu wanawake wa TANESCO na wataalamu wengine wa kada hiyo kutokana na makongamano kuwa sehemu mahususi ya kuzungumzia masuala ya kada ya husika.

 Â
More Stories
TPTC kuendelea kuendesha kozi ya ulinzi wa amani kwa Watanzania
WMA yafikia asilimia 96 utekelezaji mpango kazi wa Mwaka
Kamishna wa umeme na nishati jadidifu afanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya umeme jijini Dar