March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Wadau wahimizwa kufuata miongozo kuhakikisha usalama wa mabwawa

Judith Ferdinand, Timesmajira Online- Mwanza

Wadau na wamiliki wa mabwawa nchini Tanzania,wametakiwa kuzingatia miongozo,mipango pamoja na kufanya ufuatiliaji na tathimini ya hali ya mabwawa muda wote.

Ambapo kwa sasa nchini Tanzania kuna takribani  mabwawa 700 maeneo mbalimbali pamoja na  mabwawa ya taka sumu takribani 60 huku tathimini ya hali ya  usalama kwa sasa ikionesha kuwa mabwawa hayo yapo vizuri hayana viatashiri.

Mkurugenzi wa Huduma za Ubora wa Maji kutoka Wizara ya Maji,Mteki Chisute, akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufungua mkutano wa mwaka wa usalama wa mabwawa unaofanyika kwa siku tatu mkoani Mwanza

Wito huo umetolewa Novemba 19,2025 na Mkurugenzi wa Huduma za Ubora wa Maji kutoka Wizara ya Maji,Mteki Chisute,wakati akifungua mkutano wa mwaka wa usalama wa mabwawa unaofanyika kwa siku tatu mkoani Mwanza.

Chisute amesema,endapo taasisi mbalimbali na watu binafsi watazingatia miongozo na kuweza  kuaanda mipango ambayo itawezesha kukabiliana na hatari mbalimbali ambazo zinaweza kujitokeza katika mabwawa itasaidia kuchukua hatua kwa haraka na nchi kubaki salama.

“Kwa maana unapofanya tathimini  ni rahisi kugundua kama kuna kihatarishi chochote juu ya usalama wa mabwawa na kuchukua hatua za kuzuia hatari hiyo.Hivyo pamoja na faida za mabwawa wadau mbalimbali na wamiliki  mnapaswa kuhakikisha mnaweka  mipango mahususi ya kuhakikisha hakuna  kihatarishi chochote kinachoweza kuhatarisha usalama wa mabwawa yetu,”amesema Chisute.

Sanjari na hayo Chisute, amesema Serikali imefanya jitihada mbalimbali katika kuhakikisha inatumia teknolojia mpya kwa ajili ya uimara wa mabwawa na kuhakikisha yanadumu kwa muda mrefu.

Ambapo imeweza kununua mitambo mbalimbali kwa ajili ya kuwezesha mradi wa uchimbaji wa mabwawa na ujenzi wake pamoja na kuwajengea uwezo wataalamu na wamiliki ili waweze kufanya usimamizi.

“Baada ya kupata mitambo  katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu kuna mabwawa yamejengwa kwa ukubwa tofauti yakiwemo mamkubwa,ya kati na madogo,hiyo yote ni  kuwa na mabwawa mengi,kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya maji na kuhifadhi taka sumu ili isije kuingia kwenye mazingira na kuleta athari,”amesema Chisute.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha  Wachimbaji Tanzania(Tanzania Chamber of Mines), Mhandisi Benjamin Mchwanpaka, akizungumza baada ya ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa usalama wa mabwawa unaofanyika kwa siku tatu mkoani Mwanza

Kwa upande wake,Ofisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha  Wachimbaji Tanzania(Tanzania Chamber of Mines), Mhandisi Benjamin Mchwanpaka,amesema, kila mradi unapoanza lazima wafuate taratibu za kutathimini athari za mazingira na kuweka mpango wa kuhakikisha bwawa  la maji au sumu linakuwa limekidhi vigezo na kufuata vibali vyote kutoka taasisi zinazohusika  ikiwemo idara ya maji  na Tume ya Madini.

“Wakaguzi  hutembelea migodi mara kwa mara ili kuhakikisha mabwawa ya kuhifadhia taka yanadhibitiwa ipasavyo,endapo kutatokea tatizo la nyufa au dalili zozote za hatari mifumo ya ufuatiliaji inatambua mapema ili hatua za haraka zichukuliwe na kulinda watu,mali na mazingira  dhidi  ya madhara yanayoweza kusababishwa na taka zinazohifadhiwa kwenye mabwawa hayo,”amesema Mhandisi Mchwanpaka.

Amesema hakuna mgodi unaoruhusiwa  kutiritisha maji yenye kemikali au taka kwani ni  uchafuzi wa mazingira na kufanya hivyo ni kinyume na Sheria.Hivyo  wanaendelea kuhamasisha migodi kufuata Sheria za nchi na mamlaka husika kusimamia utekekalezaji wake.

Mkurugenzi wa Tafiti za Mazingira kutoka NEMC,Dkt.Menan Jangu,akizungumza baada ya ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa usalama wa mabwawa unaofanyika kwa siku tatu mkoani Mwanza

Naye Meneja wa Ufungaji wa Mgodi(Mine Closeru Manager) wa Mgodi wa Barrick-Buzwagi Gold Mine,Zonnastaal Mumbi,amesema mgodi huo umeweka nguvu kuhakikisha usalama wa mabwawa katika maeneo ambayo wanafanya kazi kwa kulinda wafanyakazi na jamii inayowazunguka.

Ambapo wanavyanzo vya kukusanya na kuhifadhi maji ili yasiharibu mazingira pia wanayo mifumo kwenye mabwawa hayo inayotoa taarifa ya kiwango cha maji kinachotokea na ubora wake ili kuhakikisha  hayaendi kuleta madhara katika mazingira.

Haya hivyo Mkurugenzi wa Tafiti za Mazingira kutoka NEMC,Dkt.Menan Jangu,amesema kuna aina mbili za mabwawa moja ni yakutunzia maji na mengine ni ya kutunzia  taka sumu kwenye migodi.

Hivyo ametaadharisha kuwa endapo mabwawa hayo hatayazingatia  taratibu zilizopo yatasababisha athari kwa jamii na mazingira.

“Bwawa la maji kama  halikujengwa kwa kuzingatia taratibu zilizopo   likibomoka maeneo yaliyo chini  yataathirika ikiwemo makazi na watu kutapoteza maisha.Pia mabwawa ya kutunzia tope sumu kama kwenye migodi mifumo yake isipokuwa sawa,sumu itaenda kwenye vyanzo vya maji na mashamba na kuleta athari,”amesema.

Meneja wa Ufungaji wa Mgodi(Mine Closeru Manager) wa Mgodi wa Barrick-Buzwagi Gold Mine,Zonnastaal Mumbi,akizungumza baada ya ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa usalama wa mabwawa unaofanyika kwa siku tatu mkoani Mwanza
Baadhi ya washiriki mkutano wa mwaka wa usalama wa mabwawa unaofanyika kwa siku tatu mkoani Mwanza