Na Mwandishi wetu, Timesmajira Online
Shirika la Msalaba Mwekundu (Red Cross Tanzania) pamoja na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania(TPA),limetoa misaada ya vifaa saidizi kwa ajili ya kuendelea kusaidia katika zoezi la uokoaji linaloendelea, baada ya jengo la ghorofa kuporomoka eneo la Congo na Mchikichi Kariakoo Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam.

Hivyo Naibu Waziri,Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu,Ummy Nderiananga amewashukuru wadau hao,Novemba 19, 2024.Ambapo amesema miongoni mwa vifaa vilivyokabidhiwa ni pamoja na machela 9,mashuka 100 kutoka Red Cross Tanzania, na TPA,reflectors pamoja na cover white.
Aidha alitoa rai kwa wadau mbalimbali kuendelea kujitokeza kuchangia huku akipongeza namna zoezi la uokoaji linavyoendelea kwa kushirikiana na wadau.


More Stories
Simbachawene:Mfumo wa Tathmini ya Mahitaji Rasilimaliwatu umebaini upungufu wa watumishi 441,366
Wakazi Arusha watakiwa kuchangamkia fursa huduma jumuishi za kifedha
Wahitimu wa Mafunzo ya Scout Nkasi watakiwa kuwa mwangaza kwa vijana