Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online, Simiyu
SHEKHE Mkuu wa Mkoa Wa Simiyu Mahamud Kalokola amesema Hayati Rais John Magufuli alifanya mengi hasa kwa Watu wanyonge ambao kwa kiasi kikubwa alikuwa akiwatetea.
“Hayati Rais Magufuli amefanya Mambo makubwa, alikuwa mtetezi wa wanyonge. Kikubwa tumuombe huko aliko mungu ampunguzie adhabu ya kaburi” amesema Shehe Kalokola.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga amesema Hayati Rais Magufuli alijipambanua kuwa mtetezi wa wanyonge na kwamba ni vema Watanzania wakaendelea kunuenzi na kumkumbuka kwa mema aliyoyafanya.
Ibada hiyo maalum ilifanyika katika Viwanja vya CCM Wilayani Bariadi Mkoani Simiyu Na kwamba iliandaliwa na Chama Cha Mapinduzi.
Aidha, Viongozi wa dini wakiwemo wa Kanisa Katoriki, KKKT, Kanisa la Halisi la Mungu Baba, Kanisa la Wasabato.

More Stories
Serikali yafikia asilimia 90 ya usambazaji umeme Vitongoji Kilimanjaro
Asenga ahoji utaratibu wa kufuata kwa wanaofanya biashara barabarani
Mhandisi Ntemi ahoji upatikanaji gari zimamoto Katoro