Na Penina Malundo, TimesMajira Online, DSM
VIONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wameondoka Ofisi za Makao Makuu wamewasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), kumpokea Makamu Mwenyekiti wa Chama Taifa (Bara) . Tundu Lissu .
Lissu atatua uwanjani hapo saa 7.20 mchana huu. Baada ya kupokelewa JNIA, Makamu Mwenyekiti huyo ataelekea Ofisi za Makao Makuu ya Chadema, Mtaa wa Ufipa, jijini Dar es Salaam, ambako atazungumza na Waandishi wa Habari.
More Stories
Lulida ataka viwanda vilivyofungwa vifufuliweÂ
Wizata ya Viwanda yapongezezwa kasi mageuzi kiuchumi
Bajeti ya Trilioni 2.4 uboreshaji Elimu yapitishwa Bungeni