Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
UMOJA wa Wanawake Kata ya Kimara Wilaya ya Ubungo, chini ya Mwenyekiti wake Mwajuma Ramadhani, wamefanya kikao Chake cha Baraza la Kikanuni kwa lengo la kuendelea mikakati ya Uchaguzi wa Serikali ya Mitaa.
Katika kikao hicho kilichofanyika Julai 28 mwaka huu mgeni Rasmi alikuwa Mwenyekiti CCM Kata ya Kimara, Bosco Bugali akiongozana na Diwani wa Kata hiyo Arch. Ismail Mvungi na Diwani viti Maalum, Nuru Mbezi.
Agenda Kuu katika Baraza hilo ni kuendelea na mikakati kulelekea katika chaguzi za Serikali ya Mitaa.
Akizungumza katika kikao hicho mgeni rasmi, Bosco Bugali aliwaelezea Wajumbe wa Baraza hilo mambo mengi ya kuyaishi na kuyaendea katika Maisha binafsi na Siasa ili kuimarisha CCM.
Licha ya Mipango mikakati ya uchaguzi, Diwani waKata ya Kimara aliwapongeza wajumbe wa Baraza hilo kwa mikutano mikuu ya matawi yaliyofanyika kwa mafanikio makubwa.
Hata hivyo Diwani huyo hakuacha kuwapa zawadi viongozi wote wa Baraza hilo, kwani siku zote Mcheza Kwao hutunzwa.
More Stories
Benki ya NMB yapiga jeki Zahanati ya Kijiji cha Ivilikinge Wilyani Makete
Wanawake, vijana watakiwa kuchangamkia fursa za zabuni
CCM Zanzibar yapongeza hotuba ya Dkt. Rais Samia