GAZA, Serikali ya Israel imefanya mashambulizi ya anga katika Ukanda wa Gaza baada ya wanamgambo wa Kipalestina kurusha maputo yenye vilipuzi Kusini mwa Israel.
Hali hiyo imetokea yakiwa ni makabiliano ya kwanza kati ya pande hizo mbili tangu kuzuka mzozo mkubwa mwezi Mei, mwaka huu ambapo mamia ya watu waliuawa.
Mashambulizi hayo ni ya kwanza chini ya serikali mpya ya muungano inayoongozwa na Waziri Mkuu, Naftali Bennett, aliyechukua nafasi hiyo Jumapili baada ya kuondolewa kwa waziri mkuu wa zamani, Benjamin Netanyahu.
More Stories
Wananchi Ikungi watakiwa kutumia mtandao kwa manufaa
UWT yalaani shambulio la kudhuru mwili Mwenezi BAWACHA
JAB :Kazi ya ukamilishaji wa mfumo wa kidigitali wa usajili wa waandishi wa habari inaendelea