September 30, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Mkurugenzi mkuu wa kampuni ya uelendelezaji wa Jotoardhi (TGDC) Mhandisi Kato Kabaka kushoto katika eneoe la mradi akiteta jambo na Mjiolojia Mwandamizi na meneja mradie ,Albano Mahecha

TGDC yaanza kufanya utafiti wa awali uzalishaji wa umeme

Na Esther Macha, timesmajira,Online ,  Rungwe

SERIKALI kupitia kampuni ya Uendelezaji wa nishati jadidifu ya Jotoardhi Tanzania (TGDC )imeanza hatua za awali za utafiti wa kuanza utekelezaji wa mradi wa kuzalisha Megawati 200 za umeme kwa  kupitia nishati ya Jotoardhi katika Mikoa ya Mbeya na Songwe.

Imelezwa kuwa jotoardhi ni chanzo cha nishati  kinachotumia  joto lililopo chini ya uso wa dunia .

Akizungumza na waandishi wa habari wa Mikoa ya Mbeya na Songwe , mjiolojia Mwandamizi na Meneja mradi ,Albano Mahecha amesema mradi wa  Jotoardhi wa Kyejo Mbaka uliopo Halmashauri ya ya Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya ndiyo mradi wa kwanza kuanza kucholongwa visima  kwa ajili  ya uzalishaji wa nishati hiyo uliopo Halmashauri ya Busokelo wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.

Mahecha amesema kuwa mradi huo ulianza kutekelezwa machi 3, mwaka huu na kwamba utekelezaji  mpaka sasa kwenye shimo la kwanza  wamefikia mita 70 na unatekelezwa na kampuni ya uendelezaji wa mradi wa Jotoardhi (TGDC)kwa kushirikiana na STAMICO ambayo nayo ni kampuni ya umma.

“Kiufupi lengo la mradi huu ni mwendelezo wa tafiti ambazo tunaendelea nazo tulianza na tafiti za juu na sasa tunaenda kuthibitisha tafiti za chini na kuangalia uzalishaji tunaotarajia  wa mradi na kuwisha taarifa za ziada kuwepo wa uzalishaji mradi wa Kyejo _Mbaka ,mradi unaendelea vizuri na unahusisha mashimo matatu  ya  visima vifupi  na mradi huu tunatarajia tutautekeleza na kuukamilisha ndani ya   miezi mitatu”amesema Mahecha.

Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Kampuni ya uendelezaji wa Jotoiardhi (TGDC)Mhandisi ,Kato Kabaka amesema kuwa miradi hiyo nishati jotoardhi inatekelezwa eneo la Ziwa Ngosi,Mto Songwe na Kyejo Mbaka uliopo wilayani Rungwe katika Halmashauri ya Busokelo.

Aidha Mhandisi Kabaka amesema kuwa ucholongaji ni sehemu ya utafiti kujua kwamba walichofikiria katika utafiti wa awali ndivyo kilivyo na bahati nzuri walivyochoronga wamekuta maji ya moto kwenye kina kifupi  na uchorongaji unaendelea.

Amesema kuwa shughuli inayoendelea ni kuthibiti maji ya moto ili kazi iweze kuendelea na wataalam wa kuthibiti maji ya moto tayari wapo na vifaa na kazi.

 Naye Mkurugenzi wa maendeleo wa Biashara (TGDC) Mhandisi Shakiru Kajugus amesema kuwa  mradi huo wa visima vitatu umefikia awamu  ya kutekeleza zoezi linaloendelea katika mradi huo  ni utafiti wa awali wa  mradi  unaoendelea wa kupata kiwango sahihi cha uwingi wa jotoardi katika maji na uchorongaji wa visima .

Waandishi wa Habari wa mkoa wa Mbeya na Songwe ni miongoni mwa wadau wa kwanza ambao wamepata fursa ya kutembelea miradi hiyo, kwalengo la kuhabarisha umma juu ya uwepo wa miradi hiyo nchini.