March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

TASAC:Sekta ya bahari ndiyo unayoongoza kwa mchango mkubwa kiuchumi

Na Mwandishi wetu,TimesmajiraOnline

MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Mohamed Salum amesema sekta ya bahari ndiyo inaongoza kwa mchango mkubwa kiuchumi hasa katika shughuli za usafirishaji.

Salum ameyabainisha hayo alipotembelea katika Banda la Taasisi hiyo lilipo katika maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba yanayoendelea.

Amesema sekta hiyo inazofursa nyingi ambazo wananchi wamekuwa hawazifahamu ikiwemo maeneo ambayo wanaweza kusoma na kupata ajira kwa urahisi zaidi.

Hivyo aliwaomba wananchi  kutembelea katika  Banda TASAC lililopo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba ili  waweze kufahamu sekta ya bandari na mchango wake katika uchumi.

“Tunawakaribisha watu  waje  kutembelea banda letu ili waweze wafahamu na kujua kuna fursa gani katika sekta ya bahari . Nchi yetu ya  Tanzania inaupungufu mkubwa wa wataalamu kupitia  sekta hii zipo  ajira na fursa mbalimbali nyingi.

“Duniani kote kuna upungufu wa mabaharia kwa mujibu wa takwimu za uhitaji mabaharia hawajawahi kutosha kwenye Meli”

Aidha amesema Taasisi hiyo inayo majukumu mbalimbali ikiwemo majukum  Udhibiti wa usafiri majini pamoja na kuchagiza sekta usafiri nchini .

“Jukumu kubwa la TASAC ni Udhibiti shughuli za usafirishaji majini kwa kuusajili vyombo vinavyojengwa nchini na kuvikagua kila hatua na kuvipa vyeti vya ubora”amesema Salum

Pia amesema wamekuwa wakifanya ukaguzi wa mara kwa mara wa vyombo pamoja na ukaguzi wa meli za kimataifa zinazokuja nchini.