Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online, Mbeya

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) kupitia idara ya masoko, limeendelea na kampeni kabambe ya kuhakikisha inatoa elimu kwa wachimbaji wadogo, kati na wakubwa wa madini pamoja na mashine za kusaga nafaka mkoani mbeya ili wafahamu elimu ya matumizi Bora ya umeme.
Lengo la kampeni hiyo Ni kuhamasisha matumizi bora ya umeme, usalama wa umeme kwa viwanda hivyo, kuunga mkono jitihada za Mh Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuhakikisha uchumi wa viwanda unafikiwa kwa Kasi nchini na kuongeza Tija kwa Taifa.
Miongoni mwa migodi ambayo imekwishatembelewa mkoani Mbeya ni pamoja na mgodi wa makaa ya Mawe Kiwira, mgodi wa dhahabu Chunya wa Mdimi investment, Mehrab minerals resources, mgodi wa mama Today iliyoko wilayani Chunya.


More Stories
Mgao wa tenda wa 30% kwa makundi Maalum ,wamkosha Rais Samia
Biteko ateta na Mtendaji Mkuu wa Rashal Energies, inayojenga Bomba la Gesi Kisemvule – Mbagala
Utafiti na Teknolojia matibabu ya magonjwa adimu wasisitizwa