June 6, 2025

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Sheikh Ponda kutua rasmi Act Wazalendo

Na Penina Malundo,Timesmajira 

Katibu  wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania ,Sheikh Ponda Issa Ponda kujiunga rasmi  na Chama cha Act Wazalendo  leo ambapo ni mara ya kwanza kwake kujiunga na Chama cha siasa nchini Tanzania .

Mamia ya wanachama wa  Chama hicho pamoja na watanzania mbalimbali wameweza kuhudhuria mapokezi ya Sheikh Ponda katika Ofisi za  Chama hicho Makao Makuu Magomeni Jijini Dar es Salaam. 

Mapokezi hayo ya Sheikh Ponda yameongozwa na  Kiongozi wa Chama hicho Dorothy Semu pamoja na viongozi wengine  waandamizi wa Chama hicho pamoja na Ngome zake .

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Chama hicho Ado Shaibu amesema wamefurahia sana na ujio wa Sheikh Ponda katika chama chao kwani kila jambo linawakati wake.

Amesema Sheikh Ponda anafahamika kwa mengi katika uwanja wa siasa na jina lake sio ngeni kwani kuna nyakati alipanda katika majukuwaa mbalimbali ya kisiasa ikiwemo Chama cha Wamanchi CUF pamoja na Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA.