Na. Israel Mwaisaka, TimesMajira Online, Sumbawanga
Serikali imewataka wananchi kutouza vifaa vya msaada walivyopatiwa kufuatia maafa ya upepo mkali uliosababisha nyumba 45 kuezuliwa na baadhi kubomoka katika kijiji cha Tamasenga kata ya Pito wilaya ya Sumbawanga mwaka jana.
Kauli hiyo ya serikali imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga leo wakati akikabidhi msaada wa vifaa vya kibinadamu vilivyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu Idara ya Menejimenti ya Maafa kufuatia kuathirika na upepo mkali hapo Desemba 16, 2022.

Akizungumza kwenye hafla ugawaji wa vifaa hivyo, Sendiga alionya kuwa wananchi watakaobainika kuuza vifaa hivyo wajue wanaikosea serikali hivyo itachukua hatua kali za kisheria kwa kuwa vifaa hivyo lengo lake na kusaidia kaya zilizoathirika.
Sendiga alitaja vifaa vitakavyokabidhiwa kwa wahanga kuwa ni mahindi tani 9.2, ndoo 223, mikeka 200, magodoro 200, blanketi za wakubwa 200, sahani 256, vikombe 256 na sufuria 220.

More Stories
Ndoto zilizovunjika: Jinsi Mimba za utotoni zinavyowakatisha Wasichana elimu nchini Rwanda,Tanzania na Sudan Kusini
Miaka 50 ya Sabasaba Vodacom yadhihirisha kuchochea mageuzi ya kidigital nchini
Milioni 750 kukamilisha kituo cha afya