Na Mwandishi Wetu, Timesmajira
Hatimaye Mahakama ya Moshi Mkoani Kilimanjaro mchana huu imemuachia huru aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya baada ya muda mfupi uliopita kukiri makosa yake yaliyokuwa yakimkabili.
Sabaya amekiri makosa yake kwa njia ya ‘plea bargaining’ ambao ni mchakato wa makubaliano/maridhiano maalumu katika kesi ya jinai kati ya Mwendesha Mashtaka na Mshitakiwa ambapo Mshitakwa anaweza kukubali kukiri kosa moja au zaidi katika makosa aliyoshitakiwa nayo ili apate nafuu katika kesi inayomkabili

More Stories
Wanawake jumuia ya kikristo Tanzania CCT wafundana kuelekea siku ya Wanawake Duniani
Dkt.Tulia,Mwalunenge waungana kutatua changamoto ya barabara
TUCASA yaomba kuanzishwa sheria malipo sekta ya ujenzi