Na Mwandishi Wetu, Timesmajira
Hatimaye Mahakama ya Moshi Mkoani Kilimanjaro mchana huu imemuachia huru aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya baada ya muda mfupi uliopita kukiri makosa yake yaliyokuwa yakimkabili.
Sabaya amekiri makosa yake kwa njia ya ‘plea bargaining’ ambao ni mchakato wa makubaliano/maridhiano maalumu katika kesi ya jinai kati ya Mwendesha Mashtaka na Mshitakiwa ambapo Mshitakwa anaweza kukubali kukiri kosa moja au zaidi katika makosa aliyoshitakiwa nayo ili apate nafuu katika kesi inayomkabili
More Stories
Sheikh Ponda akabidhiwa kadi ya heshima ya Maalim Seif
Sheikh Ponda kutua rasmi Act Wazalendo
Puma Energy Yazindua Mradi wa Umeme wa Jua kwa Kiwanda cha Alliance One