
Na Iddy Lugendo, Timesmajira Online DSM
KLABU ya Yanga imemtangaza MIGUEL ANGEL raia wa Argentina GAMONDI kuwa Kocha mpya wa klabu hiyo akichukua nafasi ya Nasriddine Nabi ambaye ameondoka baada ya msimu uliopita.
Miguel ana uzoefu na soka la Afrika kwa kufundisha Wydad Casablanca, Esperance de Tunis, Mamelodi Sundowns, ASEC Mimosas, USM Alger na Timu ya Taifa ya Burkina Faso.
Baadhi ya mafanikio yake akiwa Afrika ni kufika Nusu Fainali CAF Champions League msimu wa 2020|21 akiwa Kocha wa Wydady Casablanca
Msimu wa 2005|06 aliipa Mamelodi Sundowns ubingwa wa Ligi ya Afrika Kusini.

More Stories
Bilioni 7 kuwainua vijana 308 sekta ya uvuvi
Clara:Miaka 50 ya Sabasaba fursa mpya za Biashara na Uwekezaji
Usajili wa Laini za Simu: Jilinde Dhidi ya Kutumiwa Vibaya kwa Utambulisho Wako