Na Mwandishi Wetu,Timesmajira
RAIS Samia Suluhu Hasan, anatarajia kuhudhuria Mkutano wa 44 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) utakaofanyika Agosti 17, 2024 mjini Harare, Zimbabwe.
Rais Dkt. Samia anaondoka nchini leo Agosti 15, 2024
kuhudhuria Mkutano huo wenye kauli mbinu: “Kukuza ubunifu ili kufungua
fursa za ukuaji wa uchumi na maendeleo endelevu kuelekea SADC yenye
viwanda.”
Katika Mkutano huo, Rais Dkt. Samia anatarajia kuchaguliwa kuwa
Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC akipokea kutoka
kwa Rais wa Jamhuri ya Zambia Hakainde Hichilema anayemaliza muda
wake.

More Stories
TAMWA yakumbusha jamii kupinga ukatili wa kijinsia kuelekea siku ta wanawake Duniani
Wanawake washauriwa kuchangamkia fursa za uchumi
Aida:Wanawake wakipata haki zote itapunguza migogoro