Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Dr. James Peter Mataragio kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati akichukua nafasi ya Athumani Selemani Mbuttuka ambaye uteuzi wake umetenguliwa na atapangiwa kazi nyingine.
Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu imeeleza kuwa Dr. Mataragio aliwahi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania.

More Stories
Ussi awataka wananchi Handeni kulinda miundombinu ya maji
Wapambe waanza rafu za uchaguzi Morogoro Mjini
Daraja la J.P.Magufuli kuzinduliwa Juni 19,2025