Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Rais Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania itatenga eneo la ekari 20 katika mkoa wa Pwani kwa ajili ya kuhudumia mizigo kutoka Zambia.
Rais alitoa kauli hiyo wakati akitoa hotuba kwenye maadhimisho ya miaka 59 ya Uhuru wa Zambia ambapo yeye alikuwa mgeni rasmi.
Zambia ni mteja mkubwa wa bandari ya Dar es Salaam, ikichukua asilimia 34 ya mizigo yote inayopitia bandari hiyo kwenda nje ya Tanzania.
Rais Samia alitumia fursa hiyo kusema kwamba mipaka ya kijiografia baina ya Tanzania na Zambia haipaswi kuwa kikwazo cha biashara na uwekezaji baina ya nchi jirani.


More Stories
TMDA yajivunia kuanzisha mfumo thabiti wa udhibiti wa vifaa tiba na vitendanishi
Kikwete kuungana na marais watatu kushiriki Kongamano la nane la viongozi Afrika
Katavi yazindua kampeni kukabiliana na udumavu