Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
RAIS John Magufuli amefanya uteuzi wa viongozi watatu, ikiwemo kumteua Rais Mstaafu wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe.
Dkt. Shein anachukua nafasi ya Jaji Mstaafu Barnaba Samatta ambaye anamaliza muda wake.
Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi, imewataja wengine walioteuliwa kuwa ni Dkt. Harrison Mwakyembe ambaye ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS).
Dkt. Mwakyembe anachukua nafasi ya Mariam Mwaffisi ambaye amemaliza muda wake.
Aidha, Rais Magufuli amemteua, Gaudentia Kabaka kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM). Kabaka anashika wadhifa huo kwa kipindi cha pili baada ya kipindi cha kwanza kumalizika.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo uteuzi wa viongozi hao umeanza jana.

More Stories
Mfanyabiashara,vibarua mbaroni wakituhumiwa kuchimba mahandakiÂ
Silinde azindua baraza la sita la Wafanyakazi Tume ya Taifa ya Umwagiliaji
NMB ilivyosaidia Serikali kukusanya zaidi ya Sh trilioni 9.8