Fresha Kinasa, TimesMajira Online Mara.
MBUNGE wa Jimbo la Musoma Vijijini Mkoa wa Mara Prof.Sospter Muhongo ameipatia Kamati ya ujenzi ya Mmahare Sekondari mifuko 50 ya Saruji Kati ya mifuko 155, aliyochangia kwenye Harambee ya ujenzi wa shule hiyo hivi karibuni, ambayo ni shule ya tatu ya kata ya Etaro.
Amesema, Wakiimaliza ipasavyo Saruji hiyo,anaongeza mifuko mingine, huku pia akipongeza Kijiji hicho cha Mmahare kwa Kasi nzuri ya ujenzi huo ambapo tayari kimetumia mifuko yote 150 ya Saruji aliyoitoa awali katika Kijiji hicho na Vijiji vyote vinavyojenga Sekondari mpya ambapo kila Kijiji kilipata mifuko 150. Na Fedha zilizonunua Saruji hiyo ni zile za Mfuko wa Jimbo.
Hayo yameelezwa Machi 10,2025,kupitia taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Mbunge wa Jimbo hilo ambapo taarifa hiyo pia imesema kuwa ” Ujenzi wa Msingi wa kwanza wa Mmahare Sekondari ya Kijiji cha Mmahare Kata ya Etaro. Ujenzi wa msingi huo utakamilishwa leo 10.3.2025.”imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Katika harambee ambayo aliiongoza Prof. Muhongo katika Kijiji cha Mmahare, Wanakijiji walichangia mifuko 155 ya Saruji, na Mbunge huyo pia alichangia mifuko 155. Huku akitoa wito kwa Wadau mbalimbali kujitokeza kuchangia ujenzi wa Sekondari mpya 12, zinazojengwa Musoma Vijijini.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa,”Naomba kuwakumbusha kwamba hivi karibuni Mbunge wa Jimbo aligawa Saruji Mifuko 150 kwa kila kijiji kinachojenga sekondari mpya. Fedha za saruji hiyo ni zile za Mfuko wa Jimbo.Kwenye miradi yote ya ujenzi ya Jimboni mwetu, Mbunge wa Jimbo huwa anapiga harambee kuchangia ujenzi unaofanywa kwa kutumia nguvukazi na michango ya fedha za wanavijiji.”imeeleza taarifa hiyo.
Fabian Thomas ni Mkazi wa Kijiji cha M’mahare amepongeza jitihadi za Wananchi na Mbunge Prof. Muhongo, amesema zimeendelea kuleta manufaa ikiwemo kusaidia Watoto kusoma karibu na nyumbani na kuondoa changamoto ya kutembea umbali mrefu kwenda masomoni.
“Mbunge hapendi Watoto watembee umbali mrefu kwenda masomoni. Ndio maana utakuta kata moja ina Sekondari tatu hii ni kutokana na hamasa yake kwetu Wananchi. Na sisi tunashirikiana naye kwa kila hatua pamoja na Serikali yetu kufanikisha agenda ya maendeleo jimboni mwetu.” amesema Thomas.
More Stories
Mgao wa tenda wa 30% kwa makundi Maalum ,wamkosha Rais Samia
Umoja wanawake Chuo cha Magereza Kiwira watoa msaada kwa wazee
SBL yatambuliwa Tuzo za Rising Woman