Judith Ferdinand, Timesmajira Online,Mwanza
Polisi Kata ya Buleji imewataka wananchi wa kijiji cha Mwalogwabagole, Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza kuacha tabia ya kuwatumikisha watoto kwenye shughuli za kiuchumi ikiwemo kilimo na uvuvi na badala yake wawapeleke shule kwa manufaa ya baadae.

Wito huo umetolewa Februari 29,2024 na Polisi Kata wa Kata hiyo ya Buleji Mkaguzi Msaidizi wa Polisi (A/Insp) Gaidon Noah alipowatembelea wananchi hao kwa ajili ya kuwapa elimu ya usalama sambamba na kuwaeleza madhara ya uvuvi haramu ndani ya Ziwa Victoria.
Noah amewahimiza wananchi kushirikiana na jeshi hilo kwa kuendelea kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu kwa usalama na maendeleo ya taifa.


More Stories
Serikali inatambua uwepo wa Watumishi wachapa kazi na uweledi
DED Mweli:Tumeweka kipaumbele kusikiliza kero za wananchi
CHAKUWAHATA wawagusa wanafunzi wa kike