Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othman Masoud Othman, Leo Machi 12, 2024, amekutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe wa Washirika wa Maendeleo kutoka Mfuko wa Rais wa Marekani (PEPFAR); Kituo cha Kinga na Udhibiti wa Maradhi cha Marekani (CDC); na Shirika la Umoja wa Mataifa Linaloratibu Masuala ya UKIMWI Duniani (UNAIDS).
Washirika hao wa Maendeleo ambao wamefika kwaajili ya kujitambulisha na kueleza Umuhimu wa Utaratibu wa Mataifa Duniani kote, wa Kuwa na Mipango Endelevu ya Maradhi ya UKIMWI; sambamba na Kutafakari Njia Bora za Kupambana na Kuutokomeza Ugonjwa huo ifikapo 2030 hapa Nchini, wamekutana hapo katika Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Migombani, Mkoa wa Mjini-Magharibi, Unguja.
Viongozi mbali mbali wameshiriki katika Mkutano huo wakiwemo Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Harusi Said Suleiman; Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais wa Zanzibar, Fedha na Mipango, Dr. Saada Salum Mkuya; Naibu Waziri wa Afya Zanzibar, Hassan Khamis Hafidh; na Mkurugenzi Mtendaji Tume ya UKIMWI Zanzibar, Ahmed Mohamed Khatib.








👆Matukio mbalimbali katika picha
More Stories
Simbachawene:Mfumo wa Tathmini ya Mahitaji Rasilimaliwatu umebaini upungufu wa watumishi 441,366
Wakazi Arusha watakiwa kuchangamkia fursa huduma jumuishi za kifedha
Wahitimu wa Mafunzo ya Scout Nkasi watakiwa kuwa mwangaza kwa vijana