Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman, leo Januari 08 2025, amekutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe wa Kamati ya Kupambana na Udhalilishaji Zanzibar.
Ujumbe huo ulioongozwa na Mwenyekiti wake, ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar, Bi. Mwanamkaa Abdulrahman Mohammed, umefika Ofisini kwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, kwaajili ya kuwasilisha Taarifa ya Mwenendo wa Udhalilishaji Nchini, pamoja na kupata ushauri kutoka kwa Mheshimiwa Othman.
Ujumbe aliofuatana nao Bi. Mwanamkaa, umewajumuisha pia Maafisa kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka na Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar, wakiwemo Bw. Mohamed Kassim Hassan na Ostadh Abdulkarim Said Abdulla.
More Stories
Wakuu wa nchi wa EAC,SADC watoa maazimio kumaliza mgogoro wa Congo
Wanafunzi wawili waliodaiwa kutekwa wapatikana,watuhumiwa wauwawaÂ
Watumishi Madini waaswa kufanya kazi kwa bidii, kuwa wazalendo