Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA) imetunukiwa tuzo ya mshindi wa pili miongoni mwa Mamlaka za Maji nchini katika utoaji wa taarifa kwa wananchi.
MWAUWASA imetunukiwa tuzo hiyo jijini Dar-esSalaam Juni 22, 2024 na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye wakati wa kikao kazi cha Maofisa Habari Serikalini.

Tuzo hiyo imepokelewa na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma MWAUWASA, Mohamed Saif.
Mbali na tuzo hiyo, MWAUWASA imepokea cheti cha kutambua jitihada za kipekee na mikakati bunifu ya mawasiliano inayotekeleza na ambayo imeleta mchango mkubwa katika Sekta ya Habari.
Kikao kazi hicho kimeshirikisha Maofisa Habari wa Serikali zaidi ya 500 kutoka Wizara, Taasisi, Mikoa na Halmashauri mbalimbali nchini.

More Stories
COSTECH:Serikali imetenga bil.6.3 miradi ya utafiti mabadiliko ya tabia nchi
NSSF yapeleka ombi serikalini kubadilisha sheria fao la kupoteza ajira
Mabingwa Lina PG Tour 2024 kushuka dimbani kesho, michuano ya gofu Dubai