Na Bakari Lulela,TimesMajira Online
KUTOKANA na mwamko wa wanawake kujitokeza kushiriki masuala ya kugombea uongozi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, imedhihirika wakipewa nafasi, wataweza kuonesha vipawa vya hali ya juu vitakavyoleta mabadiliko chanya kwenye ukombozi wa taifa.
Hayo yameelezwa jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Chama cha Wanasheria Wanawake (TAWLA), Tike Mwambipile kwenye semina maalumu iliyokuwa ikiwajengea uwezo wanahabari namna ya kuandika ama kuripoti, taarifa zinazowahusu wanawake katika kufikia malengo yao hususan ya uongozi.
“Wanawake wana uwezo mkubwa katika kukabiliana na masuala mbalimbali ya uongozi ndani ya taifa, ambapo wakipatiwa nafasi wataweza kuleta mabadiliko chanya kwenye jamii zetu,” amesema Mwambipile.
More Stories
Kiongozi wa Mwenge awataka RUWASA kukamilisha mradi wa maji kwa wakati Kilindi
Balozi Nchimbi aongoza waombolezaji kumuaga Mzee Mongella
Ahukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa kumuua mama yake mzazi