Na Grace Gurisha
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeelezwa kuwa aliyekuwa Mhariri wa Gazeti la Mawio, Jabir Idrissa anayekabiliwa na kesi ya kuandika habari za uchochezi, yupo kwenye uangalizi Visiwani Zanzibar.
Mbali na Jabir washtakiwa wengine ni aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, aliyekuwa Mhariri wa gazeti la Mawio, Saimon Mkina na Mchapishaji wa Kampuni ya Jamana, Ismail Mehboob.
Wakili wa Serikali, Sylvia Mitanto alidai jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kuwa kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kusikilizwa, lakini mshtakiwa Jabir yupo karantini na Lissu hayupo mahakamani na hakuna taarifa zozote mpya kumuhusu.
Wadhamini wa Lissu, Robert Katula na mwenzake walikuwepo mahakamani hapo. Hakimu Simba aliahirisha kesi hiyo hadi Mei 2, mwaka huu.
More Stories
Coca-Cola Kwanza kuwanufaisha mama lishe Stendi ya Msamvu Marogoro
Sheikh Ponda akabidhiwa kadi ya heshima ya Maalim Seif
Sheikh Ponda kutua rasmi Act Wazalendo