Na Mwandishi wetu,TimesmajiraOnline,Dar
MKE wa Rais wa Jamhuri ya Finland Suzanne Innes ametembelea Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam na kufurahishwa na uhifadhi wa urithi wa asili na wa utamaduni ikiwemo fuvu halisi la mwanadamu wa kale (Zinjanthropus).
Ziara hiyo fupi iliyofanyika katika Makumbusho hayo mapema leo Mei 14, 2025 Innes aliogozwa na mwenyeji wake Katibu Mkuu Wizara ya Maliasiri na utalii , Dkt Hassan Abbas ambapo aliweza kujionea maeneo mbalimbali ikiwemo eneo ambalo limeifadhi historia kubwa ya nchi ya Tanzania
Moja ya maeneo aliyotembelea ni pamoja na kuona Utamaduni wa kitanzania, historia ya mwanadamu,pamoja na kufuraishwa na fuvu halisi la mwanadamu wa kale
Akizungumza mara baada ya kukamilika kwa ziara hiyo Katibu Mkuu Wizara ya Maliasiri na Utalii Dkt Hassan Abbas amesema wizara ya Maliasiri na utalii imekuwa na ushirikiano mkubwa na wa muda mrefu na Serikali ya Finland hasa katika sekta ya misitu na maeneo ya kubadilishana wataalamu wa misitu
“Sisi na Finland ni ndugu kabisa hata ukitembelea katika makumbusho yetu utaona picha ya hayati baba wa Taifa mwalimu Nyerere mwaka 1973 kati moja ya ziara zake alikwenda Finland”amesema Dkt Abbas
Pia amesema katika sekta ya misitu Serikali ya Finland na Tanzania zimekuwa na ushirikiano wa zaidi ya miaka 40 ambapo wamekuwa wakisaidiana katika ngazi za utaalamu .
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa makumbusho ya Taifa ,Noel Lwoga amesema kutembelewa na mke wa Rais wa Finland katika makumbusho hiyo kumeweka alama kubwa ya mafanikio ya Serikali ya awamu ya sita katika kuutagaza utalii .
Pia amesema ni alama ya mafanikio ya wizara ya Maliasiri na utalii katika kupanua wigo wa vivutio vya utalii .
“Tulizoea labda wageni wageweza kwenda mbuga za wanyama sasa wanafika katika makumbusho ni uwekezaji mkubwa ambao wizara na Serikali ya awamu ya sita imefanya katika kufungua mazao ya utalii wa Mali kale “amesema
Mkurugenzi Mkuu huyo alitumia fursa hiyo kuwaomba watanzania na wageni kutoka nje ya Nchi kuendelea kutembelea makumbusho za taifa kwa ajili ya kujifunza historia na urithi wa Taifa kufahamu utamaduni na mwingiliano wa Taifa na mataifa mengine.





More Stories
Lulida ataka viwanda vilivyofungwa vifufuliweÂ
WMA yahakiki vipimo asilimia 99 ya lengo
Rais Mwinyi:Tutamuenzi Charles Hilary kwa utendaji wake uliotukuka