Na Hadija Bagasha, Timesmajira Online -Tanga
Mgombea Udiwani Kata ya Milingano wilayani Muheza mkoani Tanga,kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mujaheed Mkadamu, Agosti 27,2025 amerudisha fomu ya uteuzi wa kugombea nafasi hiyo huku akiahidi kushughulikia tatizo sugu la maji.

Akizungumza mara baada ya kurejesha fomu hiyo, Mkadamu,amesisitiza kuwa endapo atachaguliwa, atahakikisha anashirikiana na wananchi na viongozi wa serikali kutafuta suluhisho la kudumu kwa changamoto hiyo ya maji pamoja na kuboresha huduma nyingine za kijamii kama elimu, afya na miundombinu.
Mkadamu pia amewashukuru wananchi kwa moyo wa ushirikiano na kuwataka kuendelea kudumisha amani katika kipindi chote cha uchaguzi.


More Stories
Senyamule:Serikali inapaswa kuzitambua Kampuni zinazofanya biashara ya ardhi
Serikali kuendelea kupanua fursa elimu Singida
Kumekucha CDF Cup 2026, NMB yaweka Sh milioni 150