Na Hadija Bagasha, Timesmajira Online -Tanga
Mgombea Udiwani Kata ya Milingano wilayani Muheza mkoani Tanga,kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mujaheed Mkadamu, Agosti 27,2025 amerudisha fomu ya uteuzi wa kugombea nafasi hiyo huku akiahidi kushughulikia tatizo sugu la maji.

Akizungumza mara baada ya kurejesha fomu hiyo, Mkadamu,amesisitiza kuwa endapo atachaguliwa, atahakikisha anashirikiana na wananchi na viongozi wa serikali kutafuta suluhisho la kudumu kwa changamoto hiyo ya maji pamoja na kuboresha huduma nyingine za kijamii kama elimu, afya na miundombinu.
Mkadamu pia amewashukuru wananchi kwa moyo wa ushirikiano na kuwataka kuendelea kudumisha amani katika kipindi chote cha uchaguzi.


More Stories
Kihongosi ahimiza ulipaji ada ya uanachama
Wadau wahimizwa kukomesha changamoto ya Taulo za kike shuleni
Mradi wa pamba unavyosaidia kupiga vita Ajira za Watoto