Na Mwandishi Wetu,TimesMajira Online, Mtwara
“MKINIPA kura za kutosha Oktoba 28 nawaahidi kurudisha kiwanda cha kuzalisha gasi hapa mtwara ili watoto wetu, vijana wetu nao wanufaike na rasimali hii Mungu aliyetuzawadia ”

Hiyo ni kauli ya mgombea wa urais kwa chama cha ADC Queen Sendiga alipokuwa akizungumza wananchi wakati wa kuhitimisha kampeni zake katika Wilaya Tandahimba katika kijiji cha Nanyagaa hivi ambapo sasa ataendelea na kampeni zake Wilaya ya Rufiji, Kibiti na Mkuranga.
“Jukumu lingine kubwa kwa Serikali makini inayojali maisha ya watu ni kupanga namna njema ya matumizi ya rasilimali zilizopo kwenye maeneo/mikoa husika kwa manufaa ya wakazi wake
ADC ikipata nafasi ya kuongoza nchi inaahidi kurejesha ujenzi wa kiwanda cha gesi hapa Mtwara kama Serikali ilivyoahidi wananchi wa Mtwara awali na baadae ikafanya tofauti bila kuwashirikisha

Ujenzi wa kiwanda cha kuchakata gesi kutasaidia kupunguza tatizo la ajira kwa vijana,uhakika wa umeme na upatikanaji wa gesi ya gharama nafuu kwa matumizi ya majumbani
Pia mgombea alipata nafasi ya kuwanadi madiwani wa Kata za Mdimba, Mikunda na Kwanyama
More Stories
WMA yahakiki vipimo asilimia 99 ya lengo
Rais Mwinyi:Tutamuenzi Charles Hilary kwa utendaji wake uliotukuka
Kapinga :Serikali inaendelea kutekeleza miradi ya umeme kwenye maeneo ya kimkakati