July 4, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Mgombea Uenyekiti ADC akata rufaa

Na Bakari Lulela, TimesMajira Online

MGOMBEA uenyekiti wa chama cha (ADC) Doyo Hassan Doyo amekata rufaa dhidi ya mpinzani wake katika uchaguzi wa chama hicho ulifanyika Juni 30 mwaka huu katika ukumbi wa Lamada jijini Dar es salaam.

Rufaa hiyo imekuja baada ya uendeshwaji wa uchaguzi kutawaliwa na vitimbi vya kuwakingia kifua baadhi ya wagombea Ili wawezekushinda.

Uchaguzi ambapo ulitawaliwa na sintofahamu pamoja na ukiukwaji wa Sheria na katiba za chama katika mkutano mkuu wa chama hicho.

Akizungumza jijini Doyo Hassan Doyo amesema kulingana katiba ya chama chao, uchaguzi ule ulikuwa batili kwa kuwa haukufuata kanuni, miongozo na sheria za chama.

“Uchaguzi ule ulikiuka utaratibu mzima wa kanuni na Sheria kwa msimamizi wa uchaguzi kwenda kinyume na usimamizi vilevile wapiga kura hawakupewa nafasi stahiki ya kupiga kura kwa Siri,” amesema Doyo

Doyo amesema kuwa idadi ya majina ya wajumbe yaliyokwenda kwa msajili ni machache kulingana na idadi ya wajumbe katika kinyang’anyiro cha uchaguzi huo 

Aliainisha kwa kutaja idadi stahiki ya wajumbe ilikuwa ni 192 lakini idadi ya kura zilipigwa  ni 242 ambapo imeonekana kura 50 ni batili.

MGOMBEA uenyekiti wa chama cha (ADC) Doyo Hassan Doyo akieleza kwa hisia ukiukwaji ulifanyika katika chama chake na kupelekea kukata rufaa dhidi ya uchaguzi jijini Dar es salaam.