
Na Mwandishi wetu, Timesmajira Online
Rais wa Uganda Yoweri Museveni ameonya dhidi ya kampeni zinazounga mkono haki za wapenzi wa jinsia moja nchini humo, Mapenzi ya jinsia moja ni haramu nchini Uganda.
“Usilete upuuzi wowote hapa, Tulikuwa Washington, na wakati huu Wamarekani walipanga mkutano vizuri kwa sababu hawakuleta masuala haya. Walijikita kwenye biashara, suala ambalo ni zuri. Hawakuleta masuala yeyote kuhusu wapenzi wa jinsia moja . Lakini kama wangeleta hizo mada tungekuwa na matatizo.” Rais Museveni
Ameyasema hayo Siku ya Jumatano Rais Museven alitaja haki za wapenzi wa jinsia moja kama “upuuzi” wakati wa hotuba aliyoitoa kwenye mahafali ya Chuo cha Kitaifa cha Ulinzi.
More Stories
ZOLA yajipanga kupeleka Nishati Safi kwa Watanzania, yaunga Mkono Juhudi za Rais Samia
Kiongozi wa Mwenge awataka RUWASA kukamilisha mradi wa maji kwa wakati Kilindi
Balozi Nchimbi aongoza waombolezaji kumuaga Mzee Mongella