Na Esther Macha TimesmajiraOnline,Mbeya
MKUU wa Mkoa wa Mbeya,Juma Homera amesema kuwa mpango wa msaada wa kisheria wa Mama Samia Legal Aid umerudisha furaha kwa wananchi kutokana na malalamiko na kesi nyingi kushughulikiwa kwa wakati na weledi mkubwa.
Amesema kuwa ujio wa msaada huo wa kisheria kwa mkoa wa Mbeya umeleta matokeo makubwa hususani kwenye malalamiko ya migogoro ya ardhi pamoja na ukatili wa kijinsia .
Homera amesema hayo February 24,2025 wakati wa ufunguzi wa Samia Legal Aid Campaign ambayo imefanyika katika viwanja vya Stendi ya Kabwe Jijini Mbeya na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na viongozi wa dini na kimila.
“Tumeona matokeo yake na mmeona jinsi wananchi walivyojitokeza kwa wingi hapa watu Wana matatizo, ndo maana yake jambo hili ni muhimu na mtambuka kwa wananchi wa Jiji la Mbeya hivyo tumpongeze Rais Samia kwa ubunifu huu mkubwa alioanzisha wa mama Samia legal campaign kwani kesi nyingi zinashughulikiwa na wizara ya katiba na Sheria inatimiza wajibu wake vizuri “amesema Mkuu wa mkoa wa Mbeya
Hata hivyo Homera amesema kuwa utekelezaji wa Kampeni ya msaada wa kisheria ngazi ya mkoa ilizinduliwa Jijini Dodoma April 25 ,2024 na Waziri mkuu Kasimu Majaliwa na kutoa siku 10,kusikiliza malalamiko ya wananchi na matokeo yake yanaonekana na hali ilivyo kwasasa mabadiliko ni makubwa kwa jinsi kesi zinazovyosikilizwa.
Aidha Homera amesema dhumuni kuu la msaada wa kisheria ni kuongeza uelewa wa kisheria kwa wananchi ,kuimalisha huduma ya kisheria kwa waathirika wa ukatili wa kijinsia,wanaume wenye shida mbali mbali, kutoa elimu ya usimamizi wa mirathi,utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala.
Kwa upande wake Mwakilishi wa TLS Kanda ya Mbeya,Baraka Mbwilo amesema kuwa mkoa wa Mbeya una migogoro mingi ya ardhi ambayo inatokana na sababu mbali mbali ikiwemo mwingiliano wa shughuli za kiuchumi,uzembe kwa baadhi ya watendaji wa serikali kutozingatia majukumu yao ipasavyo.
Aidha amesema pia migogoro mingine ni pamoja na mirathi ambapo wanawake hunyanyaswa na ndugu wa mume wakidhani mali zilizochumwa na marehemu ni mali yao lakini sio mali za mjane na watoto.
Faraja Nchimbi ni mjumbe wa bosi wa kitaifa ya msaada wa kisheria amesema kuwa pia kuna changamoto ya uelewa mdogo kwa makundi maalum kwa watendaji wa serikali ngazi za chini hususani ngazi za vijiji na hivyo kupelekea kutoa uamuzi unaoweza kuathiri pamoja na uwepo na Mila na desturi zilizopita na wakati.
“Ushauri wa bodi ipo haja wizara ya katiba na Sheria kuimarisha ukaguzi kwa mashirika yanayotoa huduma ngazi ya jamii ili kujiridhisha na huduma zinatolewa kwa jamii nalisema hili sababu bodi imebaini kuwa uwepo wa mashirika ya wasaidizi wa kisheria wanaotoa huduma bila kufuata matakwa ya kisheria ikiwemo kutoa huduma hizo bila kujisajili “amesema Nchimbi .
More Stories
Mwanza wahimizwa kutumia bidhaa zinazozalishwa na kampuni za kizawa
BAKWATA yashauriwa kuandaa mkakati kupata walimu wa madrasa
TEA yatenga bil.3 kufanikisha utekelezaji mtaala mpya wa elimu