Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
TAKRIBANI makanisa 84 katika miji 10 nchini Ethiopia, yamebadili rasmi mabango yao na kuandikwa jina jipya la Kanisa la Shincheonji la Yesu.Mnamo tarehe 10, Kabila la Petro la Shincheonji liliendesha tukio maalumu lijulikanalo kama “Sherehe ya Kubadilisha Mabango ya Makanisa 84 ya Ethiopia.”
Katika hafla hiyo, wachungaji 84 walitangaza kuwa wamekuwa wanachama wa Kanisa la Shincheonji la Yesu, wakiahidi kuhubiri Neno la Agano Jipya la Ufunuo na kuungana kupitia Neno lililofunuliwa.
Hayo yalitokana na ushiriki wa Mchungaji Asefa Angeto (Rais wa Jumuiya ya Denomination ya Misgana) katika “Semina ya Kimataifa ya Pili ya Ufunuo” iliyofanyika Novemba mwaka jana katika Kanisa la Shincheonji Cheongju.Hiyo imekuja baada ya kurejea Ethiopia, Mchungaji Asefa aliendelea kuendesha semina za mafundisho kulingana na Neno alilojifunza.
Mchungaji Asefa amesafiri katika zaidi ya makanisa 100 kwenye miji 10, akifanya semina na kushuhudia Neno lililofunuliwa alilojifunza kutoka Shincheonji.

Mabadiliko hayo ya mabango hayachukuliwi tu kama hatua ya kawaida ya kubadilisha majina, bali yanaonekana kama hatua kubwa ya mageuzi ya kiroho yenye msingi wa Neno ndani ya jumuiya ya Kikristo ya Ethiopia.Katika sherehe ya kumbukumbu, wachungaji 84 waliotoka kwenye makanisa hayo walisema:
“Tumekuwa wanachama wa Kanisa la Shincheonji la Yesu, tukiwa tumeshika Neno la Agano Jipya la Ufunuo.
“Tunaazimia kulihubiri Neno hili kote Ethiopia ili wachungaji na waumini wote wafuate ukweli pekee na wajitoe kwa bidii zaidi katika huduma ya Neno.”Mwakilishi wa Kabila la Petro la Shincheonji amesema

“Kwa sasa, wachungaji 181 nchini Ethiopia wanajifunza Neno lililofunuliwa kutoka Kanisa la Shincheonji la Yesu.
“Tutaendelea kutangaza kuwa unabii wa Ufunuo umetimizwa leo, na tutaweka jitihada kubwa ili makanisa kote ulimwenguni yaungane kupitia Neno.”amesema

More Stories
Wanawake jumuia ya kikristo Tanzania CCT wafundana kuelekea siku ya Wanawake Duniani
Dkt.Tulia,Mwalunenge waungana kutatua changamoto ya barabara
TUCASA yaomba kuanzishwa sheria malipo sekta ya ujenzi