March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Makamu wa Rais Dkt. Nchimbi afanya mazungumzo na Rais wa Zanzibar

Na Agnes Alcardo, Timesmajira Online. Zanzibar

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa ushindi wa kishindo aliyoupata katika Uchaguzi Mkuu, Oktoba 2025.

Makamu wa Rais ametoa pongezi hizo wakati akizungumza na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi, mazungumzo yaliyofanyika Ikulu Zanzibar, amesema, ushindi huo ni matokeo ya kazi kubwa aliyofanya Dkt. Mwinyi pamoja na Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.

Aidha kwa upande wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amempongeza Makamu wa Rais Dkt. Nchimbi, kwa kushika wadhifa huo, na kumuhakikishia kuendelea kufanya kazi kwa karibu na Ofisi ya Makamu wa Rais katika kutafuta ufumbuzi wa masuala mbalimbali ya kimuungano.

Makamu wa Rais Dkt. Nchimbi, amefanya mazungumzo na Rais huyo wa Zanzibar lengo likiwa ni kujitambulisha.