Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online Zanzibar
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Othman Masoud Othman,jioni ya leo Machi 01, 2024, amejumuika pamoja na viongozi mbalimbali katika hafla ya kuupokea Mwili wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Hayati Ali Hassan Mwinyi.

Viongozi hao ni pamoja na wa Kitaifa wa Serikali, dini na Wanasiasa Mashuhuri, Viongozi Wastaafu, Mabalozi, Wanadiplomasia, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, familia na wananchi,
Hafla hiyo ambayo imefanyika katika uwanja wa ndege wa Abeid Amani Karume Zanzibar, imeongozwa na Mgeni Rasmi, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan na kuhudhuriwa pia na Rais wa Zanzibar Dokta Hussein Ali Hassan Mwinyi.

Katika hafla hiyo, Mheshimiwa Othman ameambatana na Mke wake, Mama Zainab Kombo Shaib.





More Stories
Ussi awataka wananchi Handeni kulinda miundombinu ya maji
Wapambe waanza rafu za uchaguzi Morogoro Mjini
Daraja la J.P.Magufuli kuzinduliwa Juni 19,2025