Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othman Masoud Othman,jioni ya Septemba 1, 2024 ameitembelea na kutoa mkono wa pole kwa familia ya Almarhum Hawa Mairo,ambaye ni mama wa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Batilda-Salha Buriani, alifariki dunia,mapema Agosti mwaka huu.

Ambapo Makamu huyo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar,ametoa mkono wa pole kwa familia hiyo,nyumbani kwao marehamu huyo,Momela-Tanzanite, Wilaya ya Arumeru, Mkoa wa Arusha.

Othman yupo Jijini Arusha, kwa ajili ya ziara ya siku mbili,inayohusisha shughuli mbalimbali za jamii na serikali.

More Stories
Wanafunzi Ilala Boma wafanya ziara ya Masomo uwanja wa ndege
Nishati ya umeme jua kupunguza gharama za uzalishaji migodini
Rais Samia atoa bil.10 ukarabati barabara za ndani Ilala