Na Mwandishi wetu, timesmajira
Makamu Mwenyekiti wa ACT – Wazalendo Zanzibar ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othman Masoud Othman, leo Jumatatu Machi 04, 2024 amejumuika pamoja na Viongozi wengine Wakuu wa Chama hicho, katika Kikao cha Halmashauri Kuu, huko katika Ukumbi wa Hakainde Hichelema, Makao Makuu ya ACT- Wazalendo Magomeni Mikumi, Jijini, Dar es Salaam.

Kikao hicho cha Halmashauri Kuu, ambacho kimeongozwa na Mwenyekiti wa ACT- Wazalendo Taifa, Ndugu Juma Duni Haji, ni katika muendelezo wa vikao kuelekea Mkutano Mkuu wa Uchaguzi unaotarajiwa kufanyika tarehe 5 na 6 mwezi Machi.

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Kiongozi wa Chama, Makamu Mwenyekiti ACT Wazalendo Bara na Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Ndugu Zitto Zuberi Kabwe, Doroth Semu na Ado Shaibu Ado.
More Stories
Kituo cha afya Kisiwa cha Rukuba chafungiwa umeme jua kurahisisha huduma
Kapinga:Wakandarasi wasimamiwe kutekeleza miradi ya nishati kwa wakati
Rungwe yajenga soko kukuza uchumi kwa wananchi